Marehemu
Veronica Salehe (54), mkazi wa Kijiji cha Ikondamoyo Tarafa ya Nsimbo
Wilaya ya Mlele mkoani hapa aliyewahi kuripotiwa kuolewa na wanaume
wawili akiwa na wanaume hao.
Ameacha simanzi! Kifo cha mwanamke,
Veronica Salehe (54), mkazi wa Kijiji cha Ikondamoyo Tarafa ya Nsimbo
Wilaya ya Mlele mkoani hapa aliyewahi kuripotiwa kuolewa na wanaume
wawili tofauti na taratibu zilizozoeleka aliyeishi nao kwa kipindi cha
miaka tisa, kimeacha simanzi nzito kwa wanaume hao.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ikondamoyo, John Maganga, kifo
hicho kilichotokea hivi karibuni mkoani Tabora ambako Veronica alikuwa
amekwenda kupatiwa matibabu kwa kaka yake, kimefanya wanakijiji wa
kijiji hicho kubaki na mshtuko kwani kilikuwa cha ghafla na kwamba
wanaume hao wamepata pigo kubwa.
Mwenyekiti
huyo alieleza kuwa, katika uhai wake, aliishi vizuri na wanaume hao,
Paulo Sabuni (62) (mume mkubwa) na Arcado Mlele (47) (mume mdogo) hivyo
kuwashangaza wengi ndiyo maana kifo chake kimekuwa habari inayozungumzwa
na wengi.
Ilielezwa
kwamba, umaarufu wa Veronica kijijini hapo ulitokana na shughuli za
kilimo na biashara ya pombe ya kienyeji aina ya komoni alizokuwa
akijishughulisha nazo.
“Kiukweli
kifo chake kimewagusa wengi kwa sababu alifanya kitu cha tofauti cha
kuweza kuhudumia ndoa mbili na kila mwanaume akawa sawa bila
kuhitilafiana na mwenzake, jambo ambalo kwa wengine ilionekana kitu
kisichowezekana,” alisema mmoja wa wanakijiji hao na kuongeza:
“Hata hivyo, ndoa na mume mdogo ilivunjika mwaka jana.”
Veronica alibahatika kuwa na watoto wanne, wawili wa kike, mmoja wa kiume akiwa ni wa mume mdogo na wengine wa mume mkubwa.
Katika
shughuli za msiba wa Veronica, wanaume hao walishirikiana hadi
wakamaliza msiba huo ambapo mazishi yalifanyika kijijini hapo nyumbani
kwa baba wa marehemu, Salehe.
Comments
Post a Comment