MCHIMBAJI MDOGO WA MADINI YA TANZANITE KUTAMBULIWA RASMI KUWA BILIONEA BAADA YA KUPATA MAWE MAWILI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 7.8
Mawe makubwa mawili ya Tanzanite moja lina kilo 9.2 ambalo lina thamani ya shilingi
bilioni 4.5 na la pili lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.
Afisa Madini akionyesha moja ya jiwe la Tanzanite lilipatikanaKatibu Mkuu Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila amesema kuwa leo Wizara inamtabua Mchimbaji mdogo wa madini ya Tanzanite Bw. Saninniu Laizer kuwa bilionea baada ya kupata mawe makubwa mawili yenye thamani ya shilingi bilioni 7.8.
Katibu
Mkuu amesema kuwa mchimbaji huyo amepata mawe hayo mawili ambapo moja
lina kilo 9.2 ambalo lina thamani ya shilingi bilioni 4.5 na la pili
lina kilo 5.8 lenye thamani shilingi bilioni 3.3.
"Na
utofauti wake ni kwamba mawe ya uzito huo hayajawahi kupatikana kwenye
machimbo ya tanzanite tangu machimbo yaanze na yamepatikana ndani ya
ukuta wa Mirereni kwahiyo hii ni rekodi mpya ya kupata mawe yenye uzito
huo" amesema Prof. Msanjila
Comments
Post a Comment