Timu ya Star boys fc imewashushia kichapo cha magori
3-2 timu ya Ushirombo star ya Ntegele kwenye ligi ya Doto Cup 2019 uwanja wa michezo Kata ya Bulangwa Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita.
Wafugaji wa magori timu ya Star boys fc Daud Emmanuel dakika
ya 15 goli la pili pia Daud Emmanuel dakika ya 38 goli la tatu limefungwa na
Richard Kandolo dakika ya 63.
Aliyefuga goli la timu
ya Ushirombo star Pasi Kuya dakika ya 28 goli la pili lilifungwa na Mfaume
Mtimbe dakika ya 75 na kufikia mwisho wa
kushiriki ligi ya Doto Cup 2019 huku wenzao Star boys fc wakijipanga kukutana na
timu nyingine.
Mchezeshaji wa mechi
hiyo Magela Kilosa alisema kunawachezaji wawili wa timu ya Star boys fc wamemaliza
mchezo wanakadi za njano katika michezo yao wabadilike watakuja kupewa kadi
nyekundu huku timu ya Ushirombo star wakitoka na kadi moja ya njano.
Mshabiki wa timu ya Ushirombo star Joel Simon akilaumu
wachezaji kuwa wamefungwa kutokana na kuachia nafasi ya maadui wao upenyo huku
wakijuwa ligi hii ukipigwa ndo umetoka hadi mwakani.
Msimamizi wa ligi ya Doto Cup 2010 Kata ya Bulangwa Marco Nsolo alisema lengo
la mdhamini wa Ligi hiyo Mbunge wa jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko ni kuwaunganisha
vijana kwenye michezo na kutambua kuwa michezo ni ajira.
Comments
Post a Comment